K.O.K.W.A - 10

By: Richard Mwambe

0
Available Stock:

Ilipoishia


Yule mwingine aliyekuwa pale chini kumbe alishazinduka kitambo. Akaichomoa bastola kumwelekea Amata asijue ni mtu wa namna gani wanayepambana naye. Amata kwa haraka alimchota ngwala yulealiyekuwa akipambana naye na wakati akianguka, ile risasi ilifumua kichwa chake na Amata kwa kasi na ustadi alikirusha kisu kilichodidimia kwenye koo la yule mshenzi mwingine. Amata akaangukachinikwa kishindo huku akishuhudia wawili walewakiachana na uhai kwa maumivu makali.

“We ni Amata?” sauti ikasikika kwenye kile kifaa cha mawasiliano.

“Zamu yako inakuja, hutonikimbia...” Amata akajibu na kutoa kile kifaa sikioni akakitupa kando. Kwa haraka akaondoka kwenye ile nyumba kwa kupitia upande wa nyuma. Akakwea ukuta na kuruka nje. Katika pachipachi za nyumba ile na nyingine. Kablahajatokeza barabarani akachungulia kwanza kwenye lile jengo la Umoja ambalo yule jahili alimwambia kuwa Binusi yupo pale. Macho yake yalishuhudia Peugeot 106 ikigeuzwa kibabe na kuondoka kwa kasi. Yeye! Akawaza.


Endeleeeaaa 

View or Download Book
📘 View PDF ⬇ Download

Related Products

Product Image
K.O.K.W.A Sehemu ya 07

By: Richard R. Mwambe

Product Image
PASIPOTI YA GAIDI - Kitabu Cha 1

By: Richard Mwambe

Product Image
ISABELA - Mpango Hasi

By: Richard R. Mwambe

Product Image
Dira Ya Maendeleo 2050

By: Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania