By: Richard R. Mwambe
Kamanda Amata aliegesha gari nje ya jengo la Makumbusho ya Taifa saa tano asubuhi siku iliyofuata. Nje ya jengo hilo katika Mtaa wa Shaaban Robert shughuli zilikuwa zikiendelea kama kawaida. Akatazama harakaharaka huku na huko, na kwa sekunde hizo chache alizotazama alikwishaona vitu na mambo mengi ambayo ingekuwa wewe usingeyaona. Akavuta hatua na kuzikwe ngazi mpaka mapokezi. Katika dawati la mapokezi, alipokelewa na kijana mtanashati aliyevalia kitamaduni na kupendeza kwelikweli. “Naweza kumwona mkurugenzi Bwana Kisinini?” akamuuliza mara baada ya kumsabahi.
Jipakulie PDF yako!
By: Richard Mwambe
By: Richard Mwambe
By: RICHARD MWAMBE
By: Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania