K.O.K.W.A

By: Richard MWAMBE

0
Available Stock:

Ilipoishia…

 “Sasa kazi inaanza!” akajisemea na kuchukua bastola kutoka kwenye lile gari, akaikagua na kuhakikisha ipo sawa. Akafyatua kitasa cha mlango, akateremka na kulirudia lango. Sasa kamanda Amata alikuwa akiongozwa na hasira zaidi kuliko utashi. Akatoka nje ya uzio na kuvuta hatua kuelekea Ofisi ndogo za Bunge. Lengo lilikuwa ni kumtaka mmiliki wa hilo gari na nani alikuwa akiendesha. Aliamini kuwa hao wangeweza kumfanya ampate Braison Sambala. Na kupitia wao angeweza kuanza kuingia ndani ya hujuma na kugundua tatizo. Je wanahusika na upotevu wa Kokwa au kuna jingine? Akajiuliza.

✠ ✠

 

Endelea…

       Mchana wa siku hiyo, wafanyakazi wachache sana walikuwa katika ofisi zao. Wengi walikuwa wametoka kwa Chakula cha Mchana na wengine walienda msikitini. Amata alipanda ngazi kufika ghorofa ya kwanza ambapo alipokelewa na mwanadada mrembo aliyekuwa nyuma ya dawati la mapokezi.

         “Karibu sana kaka nikusaidie,” akamwambia Amata.

         “Asante kwa wema wako… unaonekana u mwema sana… samahani naweza kumpata mmiliki wa gari hilo hapo chini?” akauliza.

         “Lipi?” yule mwanamke akauliza.

         “Hilo Mazda!”

         “Enhe walitakia nini mi’ ndiye mmiliki…” yule mwanadada akaeleza bila kujua lengo la muulizaji. Kwa upande wa Amata.

         “Nashukuru kukufahamu, nahitaji tuongee biashara, mimi mgonjwa sana wa aina hii ya magari…” Amata akasema, “Lakini sijakujua hata unaitwa nani… mimi naitwa Jaffar,” akasema.

         “Naitwa Nuru Sembaga!”

         “Nuru… unasemaje?” Amata akauliza. Nuru alipogongana macho na mwanaume huyo aliinama chini.


Jipakulie pdf yako sasa...

View or Download Book
📘 View PDF ⬇ Download

Related Products

Product Image
PASIPOTI YA GAIDI - Kitabu Cha 1

By: Richard Mwambe

Product Image
KITANZI CHA MWISHO

By: Richard Mwambe

Product Image
KOKWA - EP 01 (Kijasho Chembamba)

By: Richard Mwambe

Product Image
ISABELA - Mpango Hasi

By: Richard R. Mwambe