By: Richard Mwambe
Ilipoishia...
Amata alielewa na alijua kuwa Mkuju
na Bahi ni maeneo muhimu sana kwa Taifa la Tanzania kwakuwa kwayo paligundulika
madini ya Urani na tayari mpaka wakati huo kule Mkuju uchimbaji wa majaribio
ulikuwa umeanza. Kuna uhusiano gani wa huyu jamaa na haya maeneo?
Akajiuliza. Na vipi kuhusu Kibaoni huko Dumila? Ninahitaji kutembelea maeneo
haya haraka iwezekanavyo! Akawaza. Kamanda Amata aliona hatua aliyofikia ya
kutafuta taarifa. Mpaka hapo aliona sasa anahitaji kuziweka pamoja taarifa hizo
hata kama ni chache, aliamini kuwa zitampa jambo kubwa. Akauendea mlango na
kutoka nje, akaurudishiakama alivyoukuta na kuondoka zake pasi na upinzania
wowote. Haiwezekani!
Endelea...
By: Richard R. Mwambe
By: Richard R. Mwambe
By: richard MWAMBE
By: Richard Mwambe